DIBAJI | HADITHI | ANWANI | MALENGO | MAISHA | PICHA | BLOGI    
       
  siku moja nilikuwa nimeenda kumtembelea rafiki yangu ambae pia ni kama mwalimu wangu wa kimaisha
rafiki yangu si wa umri wangu bali nim mzee ambae mimi naweza kuwa mtoto wake wa mbali kama vile wa
nne hivi.

Bwana huyu amewahi kunipa hadithi nyingi sana za kimaisha ambazo zataka wakati kuzisimulia lakini kwa
leo ningependa kuto kisa kidogo tu kati ya visa vingi alivyo wahi kunieleza.

Katika hali ya mazungumzo yetu ya kila siku,alinipa hadithi kama wasia pia kwa njia nyengine,je niwasia
aina gani huo?tega masikio na macho usikize ujue ni wasia gani alionipa na wewe pia uweze kuutafakari kwa
kina .

Rafiki yangu:

-aseama mtu ukiishi duniani yatakikana ufe kabla hujakufa
- ufilisike kabla hujafilisika.
- uchukiwe kabla huja chukiwa.
- upendwe kabla huja pendwa


Baada ya kuelezwa maneno haya ma nne mimi nilitatizika sana kiasi cha kumuuliza maana yake ni nini?akaniambia
niende nikatafute maana yake nije nimueleze,basi nikawa na kibarua cha kutafuta maana ya haya maneno manne,siku
moja baada ya kuhangaika sana akaniambia leo nitakueleza maana yake.

Kufa hujakufa;ni hivi,je imekupitia katika nafsi yako kuwa pengine siku moja wawezakulala na usiamke ikawa
ndio safari yako?je mfano uko na watoto au familia yako inayo kutegemea halafu litokee jambo hilo umewaekea
mti gani ambao watashikilia?

Ufilisike kabla huja filisika fikiria leo uko kazini ni ifikapo mwisho wa mweza wapata mshara wako kama kawaida
je umefikiria kuwa siku moja waweza kuenda kazini ukute notisi ya kusema wewe huduma zako hazitakiwi tena?je uki
fikiwa na hali hiyo kwa ghafla je utafanyaje?

Uchukiwe kabla kuchukiwa,mfano wewe una marafiki wengi wanakupenda sana,halafu asubuhi moja uamke ukute kila mtu
hana haja na wewe wala kukuona je ukifika hali hii utafanyaje au rafiki yako atakuwa nani?

Pendwa huja pendwa ,ni mfano wewe watu wanakuchukia sana,halafu siku moja itokee watu wawe wanakupenda sana je wewe
hali hii utaichukuliaje au utafanyaje?

kwa ufupi hadithi hii nia na madhumuni yake nikumfanya mtu awe saa zote yuko katika hali ya tahadhari awe tayari kwa lolote
litakalo tokea kwa ghafla bila kutarajia kwani hii dunia ni rangi rangile leo iko rangi hii kesho iko rangi nyengine
kwa ufupi huwa yabadilika badilika kila ukikaa ujue lolote laweza tokea.

 
     
dibaji soma hadithi kutoka ukurasa huu anwani malengo maisha picha blogi ,toa maoni yako hapa